Home Search Countries Albums

Namwachia

MAUA SAMA

Namwachia Lyrics


Yangu furaha, Imegeuka majuto
Kicheko kimegeuka kilio
Ila ninaamini wema hauozi umenipa mazito, me naumia hey
Nilijua  utanifuta machozi umenipa majonzi, me nalia
Zangu hisia nilishindwa kuficha
Wazi wazi ukatambua
Na Ndonga ukanpasua
Wangu rafiki, Wote ulowajua
Na Nguo ukawavua, Pasipo me kujua
Wacha nikae pembeni

(Namwachia Mungu tu)
Labda kuna mahali nilikosea
(Namwachia Mungu tu)
Kesi yako kwake nakushtakia
(Namwachia Mungu tu)
Maana umezidi kunionea
(Namwachia Mungu tu aaaahh)

Nilikupa Muda na vyote vilivyo vyangu
Ila malipo ya yote kunitukanisha na ndugu zangu
Kweli mzoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi
Nimelijua sawa
Moyo wangu umeuchakaza
Umehondomola mpaka gunzi
Wema umenilipa ubaya

Sitoshindwa hata tukionana
Kuachana sio uhasama
Sintothubutu kuzozana nimekunawa
Nakuombea kheri salama
Umpate yule mtakae wezana
Kumbuka kugunga zipu bwana msije kwazana
Zangu hisia nilishindwa kuficha
Wazi wazi ukatambua
Na Ndonga ukanpasua
Wangu rafiki, Wote ulowajua
Na Nguo ukawavua, Pasipo me kujua
Wacha nikae pembeni

(Namwachia Mungu tu)
Labda kuna mahali nilikosea
(Namwachia Mungu tu)
Kesi yako kwake nakushtakia
(Namwachia Mungu tu)
Maana umezidi kunionea
(Namwachia Mungu tu aaaahh)

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2022


Album : Cinema (EP)


Added By : Farida

SEE ALSO

AUTHOR

MAUA SAMA

Tanzania

MAUA SAMA  is an artist from Tanzania ...

YOU MAY ALSO LIKE