Home Search Countries Albums

Sala Lyrics


Yoh Yoh, its KK yoh
Bwana asifiwe, kikosi kazi
Prayers!

[P- Mawenge]
Hey God please help us
Tunadeal na mahaters
Wananuna wakituona vile tunashine
Tunadaka papers

Daily wanataka favours
We rap and they don't pay us
Dili la mwisho kutupa only asante
Is what they gave us

Home I got the kids men
I'm the one to feed them
Na fursa sizipati
Kila napokwenda ni competition

Still niko kwenye mission
Nishajiwekea ambition
Niweze peleka watoto 
Hospital, school and tuition

Japo vikwazo ni vingi
Basi nifanye niweze survive
Tumeshakuwa madingi 
Lord we need to be alive

Nipate kwana magimbi
Ndo nikaombe car to drive
Na nina mengi ya kukuomba 
Not 3, 4, 5

Bariki shughuli zangu zote
Niondolee mikosi
Ili nami kila weekend home
Nisherehekee kiboss

Unipe pamba niwe mjanja 
Uniongezee misosi
Baba tushachoka kila siku
Wao ndo watuonyeshee minoti

[Nikki Mbishi]
My soul soul God fearing
No goals niamini 
Hata nikiwa down
His grace hufanya re-up me

Wala sio mfear ding
Devils interfering
Sometimes nakuwa savage
Mpaka mwenyewe siamini

Lord forgive me for my sins sijui niite ndaro 
Kuna saa watakuabudu daily mbishi njaro
Shetani ananishawishi ati nishike adabu baro
Niwamalize maboss matozi sharobaro

Nagundua wewe ni upendo unapenda watu
Huniachi japo sometimes huwa nakwenda fyatu
Na-surrender kwako when I remember gospel
Umeniprotect January to December I got you

Sio kwa chanjo za Bill Gates ndo mtapona
Msijeshtuka ikiwa real late ju ya Corona
Aha yeah Mungu ibariki Tanzania
Africa mashariki na dunia
Nawasisi walotangulia
Amen

[Man-Suli]
Oh Lord, Oh Lord
Naanza kwa jina la mwingi wa rehema
Nasimama mbele zako ili niweze kusema
Na neno langu kubwa ni Alhamdullilahi
Nashukuru kwa kila neema til the day I die

Tazama hii pumzi nayo vuta
Ni maafa mangapi mja wako umeniepusha
Unaponipa riziki nasahau kukushukuru
Kinapokuja kiza ona unaniletea nuru

Dunia inanihadaa najiona mfalme mimi
Kiburi na majivuno leo naviweka chini
Kiumbe dhalili mimi, mwana wa Adamu
Tone la amani nashukuru kwa ufahamu

Siwezi jiita mwema ila najitahidi
Mengi nakosea na kutubu imenibidi
Leo siombi chochote ila tu unikumbuke
Siku ya mwisho wangu, mwisho mwema unikute

[Zaiid]
Kabla ya kupiga makofi na kuparty
Napiga magoti na kusali
Kisha namwomba God hii mikosi iende mbali
Nikitafakari kodi ju ya pesa ya halali

Duniani kuna wapuzi kibao
Naogopa ukinipa nguvu nitadeal na pumzi zao
Nipe maarifa ya kuishi na maisha
Kabla hujaniita naomba unijaze taarifa

Natamani nikuone tupige zetu mastory
We ndo unanielewa kupita yeyote homie
You can call me maana shetani kapanda mori
Deal nae umdhibiti, ka nakufuru I'm sorry

Mi ni dhaifu
Ila shetani hanitishi
Mlango hanipishi
Mi nampush kwani vipi?

[Sterio]
Nakukimbilia wewe Bwana 
Nisiaibike milele
Safari hii bado ndefu sana 
Wakufanya nifike ni wewe 

Yeah nakuomba unilinde kwenye giza
Nilinde kwenye mwanga balozi anipe visa
Nikapasue anga michongo kukimbiza
Nikanyakue namba ndoto kutimiza

Kabla ya kurudi kwenye mchanga
Yesu kristo Tumaini letu, salama yetu
Alahu Akbar, Asalaam aleikum
Afe Maria asalaam, afe mama yetu
Siabudu masanamu afe Bwana Yesu

Maadui wasifurahi kwa kunishinda
Wakinikopa wasinidai kwa kuniwinda
Bariki familia yangu kaya nzima
Nakuomba unijalie kifo chema 
Amina

[Azma]
Ambition, my vision
One mission, I listen
Sina kitu chochote cha kusimama nacho
Sijafika popote na ninakesha macho
Asante baba haujaniacha nipotee njia
Fungu la saba sijaleta nisamehe pia

Nakushukuru kwa zawadi ya uhai
Sikufuru ka huna wema haufai
Nikawa mtumwa wa "i"
I believe in You, I don't believe in lies

All I need is you
Wewe ndio jibu ya maombi yangu
Unanitibu ya moyoni mwangu
Sioni mimi ni nani au nimekupa nini?
Mbona sina imani na unanidhamini?

Maisha yangu yamejaa majaribu
Kila nachojaribu naishia kuharibu
Sijakuweka karibu 
Najua ndio sababu sipati majibu

[One the Incredible]
Nashukuru niko uhai 
Nashukuru kuwa na afya nimeshiba
Ninashukuru leo tena niko hapa
Asante umeniondolea mashaka

Nilipochelewa uliningojea hukuniacha
Ulinipa nilichohitaji, nilipohitaji
Nilipohitaji imani ya kuzingatia
Nilipokaribiwa na dhambi 

Najua sijakamilika naamini sijabadilika
Lakini kwa upendo wako kwangu shetani hatambi
Sadaka sadikia, duniani sina changu wala chochote
Zaidi ya baraka ulobarikia, karama ulo karimia
Nafsi yangu ndo chanya na hasi yangu
Nitafanya nafasi yangu nikihitajiwa

Naombea amani wote wenye hofu na uchungu
Wamwachie mwenyezi yote wasiyoweza kuyamudu
Nyakati ndio hizi na muda ni mchache
Atukuzwe muumba wa yote, kwa heshima tumfuate
Asante

[Songa]
Eeh Mungu nijalie Amen
Sala nisali na nisalie Amen
Watu mbali mbali nisisalie Amen
Iwahi kujibiwa na isikawie, Amen

Ah napiga magoti nakunja mikono
Nakuja mbele zako coz kukuomba hakuna kikomo
Nafahamu shida zipo hatuwezi funga midomo
Maskini ukileta ujinga hatuwezi kula vinono

Sijakamilika na huwa nafanya mapenzi ya bwana
Majaribu hayaniishi shetani ni mshezi sana
Eti jana kuna binti alikuja na akauliza
Ati Songa na hicho kitambi chako utawezana?

Nachofurahi umenipa uhai my Lord
Na siku na die naomba uniwahi pepo
Nipe ujasiri ukakamavu kama askari depo
Safari iwe fresh ka uvumapo kwa bahari upepo

Dear Lord, Dear Lord

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2020


Album : Sala (Single)


Copyright : (c) 2020


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

KIKOSI KAZI

Tanzania

Kikosi Kazi is a biggest HIP HOP group from Tanzania, formed by 8 members ie Azma Mponda, Nikki Mbis ...

YOU MAY ALSO LIKE