Naanza Upya Lyrics
Tabasamu langu lisikudanganye
Hapa nlipo najililia moyoni
Kikubwa ni uhai naiomba salama
Haya mapenzi yasinichanganye
Kwenye hili ushauri sitamani
Moja haikai mbili ndo imehama
Nilipofikia ni pesa peke yake itanisumbua
Acha niumwagilie moyo niuoe vitu vyake nibadili gia
Nashushia bia nasahau yalopita najiliwazia
Ila pole sana moyo najua kuna mengi umeyapitia
Na nishawasamehe waloniumiza
Waloniliza kwenye mapenzi naanza upya
Najitunza nadunduliza
Sio mbaya nikianza upya
Namshukuru mungu sasa nimetulizana (sitaki stress)
Nataka ku enjoy moyoni shwari (sina stress)
Nikazi tu na marafiki nimetulizana (sitaki stress)
Nataka ku enjoy moyoni shwari (sina stress)
Nimeamua niache kudanganya na kudanganywa
Maana skuizi mapenzi hayana mana
Niache kula nipate kunenepeana
Eti niwaze mapenzi
Na staki nijizeeshe mi bado kijana kheri
Nitafute kibarua cha kifanya
Niwe shabiki wa mpira tu bora sana tu nianze kubeti
Yule alonichiti huko washamvhiti
Analizana na ulimwengu wa mapenzi
Hayasimuliki yupo tikitiki
Amechokeana kidudu cha mapenzi
Nishasahau yalopita najiliwazia
Ila pole sana moyo najua kuna mengi umeyapitia
Na nishawasamehe waloniumiza
Waloniliza kwenye mapenzi naanza upya
Najitunza nadunduliza
Sio mbaya nikianza upya
Namshukuru mungu sasa nimetulizana (sitaki stress)
Nataka ku enjoy moyoni shwari (sina stress)
Nikazi tu na marafiki nimetulizana (sitaki stress)
Nataka ku enjoy moyoni shwari (sina stress)
sitaki stress
sina stress
WATCH VIDEO
ABOUT THIS SONG
Release Year : 2022
Album : Naanza Upya (Single)
Added By : Farida
SEE ALSO
AUTHOR
YOU MAY ALSO LIKE