Limevuja Lyrics

Oooh, oooh maya aah
(Nusder)
Si umesema mi baniani mbaya
Na uwepo wangu kwako sio dawa, haya aah
Penzi nikashona tenzi na riwaya
Kwenye moyo wako livae liwe sawa, limepwaya
Napuliza majivu maana moto siuoni
Kooni maumivu vumbi larudi machoni
Ahadi za mbivu zimebaki ndotoni
Lile penzi tulivu leo lipo kikaangoni
Imeniponza huruma kirungi
Kujitisha kumsaidia
Kumbe katoboa mtungi
Maji yananimwagikia
Penzi limevuja tena
Penzi limevuja tena
Penzi limevuja tena
Penzi limevuja tena aah
Ulisema sikiwambaza
Penzi letu ukuta wa chuma
Nikitoka kiwalaza
Utanistiri nywele za nyuma
Mara kwa mara ulilia
Kifuani umenilalia
Ukijuta unayachukia
Yale ulopitia
Eti kama mimi hujaona
Wa kufanana naye
Asa mbona hukusema
Kama ushakutana naye
Napuliza majivu maana moto siuoni
Kooni maumivu vumbi larudi machoni
Ahadi za mbivu zimebaki ndotoni
Lile penzi tulivu leo lipo kikaangoni
Imeniponza huruma kirungi
Kujitisha kumsaidia
Kumbe katoboa mtungi
Maji yananimwagikia
Penzi limevuja tena
Penzi limevuja tena
Penzi limevuja tena
Penzi limevuja tena aah
WATCH VIDEO
ABOUT THIS SONG
Release Year : 2021
Album : Definition of Love (Album)
Copyright : (c) 2021 WCB Wasafi.
Added By : Huntyr Kelx
SEE ALSO
AUTHOR
MBOSSO
Tanzania
MBOSSO Khan (real name Mbwana Yusuph Kilungi born 3rd October 1991) is an artist | ...
YOU MAY ALSO LIKE