Home Search Countries Albums

Alisema Lyrics


[CHORUS]
Alisema, alisema
Alisema nyerere alisema
Vijina wote na tuamkee
Na sasa tuanze mchaka mchaka
Alisema alisema
alisema mwalimu alisema
Vijina wote na tuamkee
Na sasa tuanze mchaka mchaka

[VERSE 1]
Nidhambi kukaa kimya
Ni Nidhambi kutokemea
Kwa maovu na ukatili unaotokea
Najaribu kukaa kimya
Ila nafsi inanisuta
Ata Usiposema na bado yatakukuta
Ni bora ukasema sasa maana
Wakati ni ukuta
vijana wamepewa Madaraka wanatukana wazee
Hivi mnadhani mtakuwa viongozi milele
Mungu yupo acha tuone huko mbele
Naona hofu imetanda
Watu wanaogopa kusema
Maisha yamekwa magumu
Naya unaogopa kusema
Acheni uwoga kuhisi mtakufa mapema
Rest in peace akwilina
Mungu akulaze pema
Kesi ya kifo chako huku bado ni lawama
Mama ananikumbusha
Watobo bado wanasoma
Mwanangu kaa kimya usije kamatwa tena
Sawa mama hii ya mwisho naapa siongei tena ila

[CHORUS]
Alisemaaaa alisema
Alisema nyerere alisema
Vijina wote na tuamkee
Na sasa tuanze mchaka mchaka
Alisema alisema
Alisema mwalimu alisema
Vijina wote na tuamkee
Na sasa tuanze mchaka mchaka

[VERSE 2]
Sio kitaani tu
Mpaka walio maofisini
Pesa imekua ngumu lawama zote kwa joni
Walimu lawama zao (zote kwa joni)
Wakulima lawama zao (zote kwa joni)
Wafanya biashara nao lawama zao (zote kwa joni)
Bodaboda bajaji noa lawama zao (zote kwa joli)
Wamachinga wavuvi nao (zote kwa joli)
Yapo mazuri anayo yafanya hongera ziende kwa joni

Mi naona anajenga sasa faida zipo mbeleni
Jua kua mpinzani sio kupinga kila kitu
Na lengo ni moja tu kuijenga nchi yetu
Hakuna mbunge wala raisi wakukuletea chakula
Kukupa kazi kisa ulimpigia kura
Ufanye kazi na ndo upate chakula
Wasikie wabongo eti mnaitaka vita
Mnaitaka vita mnaijua vita
Uliza Libya na Congo mpaka lea wanajuta
Ila isiwe sababu yakutufanya tukae kimya
Kiongozi akizingua hatumuachi tunamchana
Poleni waandishi wa habari kazi yenu imekua ngumu
Hizo ni changamoto tusikimbie majukum
Mama ananikumbusha watoto bado wanasoma
mwanangu kaa kimya  Usije kamatwa tena
Sawa mama Hii ya mwishonaapa siongei tena ila

[CHORUS]
Alisemaaaa alisema
Alisema nyerere alisema
Vijina wote na tuamkee
Na sasa tuanze mchaka mchaka
Alisema alisema
Alisema mwalimu alisema
Vijina wote na tuamkee
Na sasa tuanze mchaka mchaka
 
Uhhhmmm…..  Uhmmm.........
Uhhhmmm…..  Uhmmm.........

 

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2018


Album : Alisema (Single)


Copyright : (c) 2018, FREE NATION RECORDS


Added By : Afrika Lyrics

SEE ALSO

AUTHOR

NAY WA MITEGO

Tanzania

Emmanuel Elibariki, popularly known as Nay Wa Mitego, or simply  Mr Nay,  is a Tanzanian r ...

YOU MAY ALSO LIKE