Home Search Countries Albums

Chozi

Y PRINCE

Chozi Lyrics


Kwetu kitanda cha kamba
Si godoro si shuka ni mkeka
Kibanda chenyewe chavuja
Aaah

Nyumba yenyewe ya kupanga
Shule nako majanga
Shati viraka
Viraka

Nikiangalia haya wazazi wangu
Namwonea huruma baba
Fundi mwenza, mbeba ngeze
Usawa umemkaba

Inamuuma roho mama yangu
Mwanawe anadhalilika
Shule ni ada, mida bwada
Nguo zimeraruka

Mama pressure inapanda
Dada naye mgonjwa sana
Kaka naye kapagawa
Yuko milembe

Baba sukari imebamba
Ndugu hawana msaada
Sote tuko njia panda
Yaani mawenge

Mang'amu ng'amu
Nadondosha chozi nakufuru Mungu
Mang'amu ng'amu
Shida kwangu ndo kimbilio

Mang'amu ng'amu
Hivi lini mimi nitapata nafuu
Mang'amu ng'amu
Oooh

Mtaani naitwa Kayumba
Mara muuza karanga
Mara muokota machupa
Aaah

Kila duka deni hatujalipa
Vikoba nao watutafuta
Yaani mchaka mchaka

Ninawaza sana
Lini tutapata na sisi?
Ututoke umasikini

Inamuuma roho mama yangu
Mwanawe anadhalilika
Shule ni ada, mida bwada
Nguo zimeraruka

Mama pressure inapanda
Dada naye mgonjwa sana
Kaka naye kapagawa
Yuko milembe

Baba sukari imebamba
Ndugu hawana msaada
Sote tuko njia panda
Yaani mawenge

Mang'amu ng'amu
Nadondosha chozi nakufuru Mungu
Mang'amu ng'amu
Shida kwangu ndo kimbilio

Mang'amu ng'amu
Hivi lini mimi nitapata nafuu
Mang'amu ng'amu
Oooh

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2019


Album : Chozi (Single)


Copyright : (c) 2019


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

Y PRINCE

Tanzania

Y PRINCE is a young artiste from Tanzania. ...

YOU MAY ALSO LIKE