Home Search Countries Albums

Nitakase Lyrics


Kuna wakati tunapitia mambo magumu
Nakujiona kwamba tunayaweza wenyewe
Kuna wakati yakitulemea twalaumu
Nakukufuru Mungu kumbe ni sisi wenyewe

Kuna wakati akili na mawazo yetu
Tunakusahau wewe tunavipa kipaumbele
Sikwamba huoni haya tunayofanya si sawa
Unatutazama kwa huruma

Vipi nikushukuru kwa nämna gani nikufae
Nami ukanifanye nuru ya ulimwengu na ikang'ae
Kwa maana umesema heri mtu yule
Asiyekwenda katika shauri la wasio haki
Bali sheria yako bwana

Unitengeneze niumbie moyo safi
Unitakase nikupendeze wewe
Unitengeneze uniumbie moyo safi
Unitakase nikupendeze wewe
Bali sheria yako bwana

Najua me nikiumbe dhaifu tu basi
Basi angalau na mimi nikupendeze wewe
Nilingane na wewe hata kwa machache tu
Niwakumbushe na wengine ili wajue upo
Maana kumeharibika

Tunaangamia kwa kukosa maarifa
Hakuna upendo ule umetufundisha
Wanadamu tumebadilika tumekuwa wabaya
Tumesahau kwamba upo
Tumesahau wewe upo
Yani kama hatuoni vile

Vipi nikushukuru kwa nämna gani nikufae
Nami ukanifanye nuru ya ulimwengu na ikang'ae
Kwa maana umesema heri mtu yule
Asiyekwenda katika shauri la wasio haki
Bali sheria yako bwana

Unitengeneze uniumbie moyo safi
Unitakase nikupendeze wewe
Bali sheria yako bwana
Unitengeneze uniumbie moyo safi
Unitakase nikupendeze wewe
Bali sheria yako bwana

Vipi nikushukuru kwa nämna gani nikufae
Nami ukanifanye nuru ya ulimwengu na ikang'ae
Kwa maana umesema heri mtu yule
Asiyekwenda katika shaur la wasio haki
Bali sheria yako bwana ikang'ae

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2022


Album : Ushuhuda (Album)


Added By : Farida

SEE ALSO

AUTHOR

WALTER CHILAMBO

Tanzania

WALTER CHILAMBO  is a Gospel Singer and Song Writer from Tanzania. He was the winner at Epic Bo ...

YOU MAY ALSO LIKE