Usifurahi Juu Yangu Lyrics

Usifurahi juu yangu eeeh adui yangu
Niangukapo mimi nitasimama tena
Kumbuka niwapo gizani bwana ni nuru yangu
Hawezi kuniacha bwana mimi niangamie
Usifurahi juu yangu eeeh adui yangu
Niangukapo mimi nitasimama tena
Kumbuka niwapo gizani bwana ni nuru yangu
Hawezi kuniacha bwana mimi niangamie
Si vyema kunisema vibaya nipatapo tatizo
Shetani wampa nafasi ndani ya moyo wako
Kumbuka kwa maombi yako nitasimama tena
Na utapata baraka kutoka kwake Mungu
Si vyema kunisema vibaya nipatapo tatizo
Shetani wampa nafasi ndani ya moyo wako
Kumbuka kwa maombi yako nitasimama tena
Na utapata baraka kutoka kwake Mungu
Maana heri mtu yule ambaye kinywa chake
Ni kuwabariki wenzake na kiwaombea
Maana maneno mabaya huchafua moyo
Ukiwekwa mbali na mungu ni vyema uwe safi
Ukiona niko kwenye shida niombee
Ndoa yangu imevunjika wewe niombee
Nikifukuzwa kazini ndugu niombee
Magonjwa yananiandamaa niombee
Biashara haina faida niombee
Nikikawia kupata mtoto niombee
Nimekuwa mtoto yatima niombee
Ata nijapo kuwa mjane niombee
Ujue kwa maombi yako mimi nitasimama tena
Ujue kwa maombi yako nitabarikiwa
Ujue kwa maombi yako mimi nitasimama tena
Ujue kwa maombi yako nitabarikiwa
Ujue kwa maombi yako mimi nitasimama tena
Ujue kwa maombi yako nitabarikiwa
Ujue kwa maombi yako mimi nitasimama tena
Ujue kwa maombi yako nitabarikiwa
WATCH VIDEO
ABOUT THIS SONG
Release Year : 2016
Album : Usifurahi Juu Yangu (Single)
Copyright : (c) 2021
Added By : Huntyr Kelx
SEE ALSO
AUTHOR
YOU MAY ALSO LIKE