Home Search Countries Albums

Nimeridhia

MAUA SAMA

Nimeridhia Lyrics


Kwa goti aliingia
Nakutaka nimsamehe
Kumbe ananichora
Mapenzi yalinijia
Kwenye moyo shurba tele
Ya-radhi akanijia
Kidudu mtu shetani akayavuruga
Akaingia mashakani tukashindwana
Kidudu mtu shetani akayavuruga
Akaingia mashakani tukakwazana
Nimeamini kwenye moyo huwezi penda mara mbili
Penzi ukalitia kasoro maskini mimi
Moyo wangu sio godoro, uwe juu me niwe chini
Si kisoda kwa kokoro, nimeshindwa mimi yeah

Aaah haya nimeridhia (sawa)
Siwezi ng’ang’ania (sawa)
Aah haya nimeridhia (sawa)
Nimeshindwa mimi
Aaah haya nimeridhia (sawa)
Siwezi ng’ang’ania (sawa)
Aah haya nimeridhia (sawa)
Nimeshindwa mimi

Kweli sio siri, ilizingwa mapema
Tamu yako ya asili, ila ndani yachoma
Kheri kuwa dhahiri, maumivu kusema
Mlaghai kwa hili, nafsi yangu imenena
Nashukuru kwa kidogo, ulichonipa nimepokea
Nitabaki kwa mikogo, huyo mwengine kumngojea
Nimeamini kwenye moyo huwezi penda mara mbili
Penzi ukalitia kasoro maskini mimi
Moyo wangu sio godoro, uwe juu me niwe chini
Si kisoda kwa kokoro, nimeshindwa mimi yeah

Aaah haya nimeridhia (sawa)
Siwezi ng’ang’ania (sawa)
Aah haya nimeridhia (sawa)
Nimeshindwa mimi
Aaah haya nimeridhia (sawa)
Siwezi ng’ang’ania (sawa)
Aah haya nimeridhia (sawa)
Nimeshindwa mimi

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2022


Album : Cinema (Album)


Added By : Farida

SEE ALSO

AUTHOR

MAUA SAMA

Tanzania

MAUA SAMA  is an artist from Tanzania ...

YOU MAY ALSO LIKE