Home Search Countries Albums

Nakesha

D LOVE

Nakesha Lyrics


Moyo umekua sugu hadi maumivu yanadunda
Siogopi waongo sipokei 
Wakweli mapenzi yamenifunza
Tamu imekua chungu moyo ulifanywa punda
Hadi mizigo ya kokoto 
Ikanichosha mwili machozi nikafuta

Sio kama siogopi kuumia tatizo nishaumia sana
Mapenzi ya maharamia nikachukia ujana
Kuna muda nawaza rudia tatizo nikipenda sana
Ndo nafasi wanaitumia kuniumiza mchana

Na usiku usingizi sipati, nakesha
Usiku nalia bahati sina (Nakesha)
Bora pombe mapenzi sitaki (Nakesha)
Ya nini kuumia bora nile dawa (Nakesha)

Kila napotarajia nitafurahia 
Ndo nazisisha 
Maumivu kwa ndani mwili umekufa ganzi
Kila pendo naloingia 
Yanajirudia kunikatisha 
Nikatisha tamaa mnyonge mwana simanzi

Kama ningeliweza kuchagua
Utotoni ningeamua
Bora hata nisingeyajua
Yataniua mapenzi

Sio kama siogopi kuumia tatizo nishaumia sana
Mapenzi ya maharamia nikachukia ujana
Kuna muda nawaza rudia tatizo nikipenda sana
Ndo nafasi wanaitumia kuniumiza mchana

Na usiku usingizi sipati (Nakesha)
Usiku nalia ah, bahati sina (Nakesha)
Bora pombe mapenzi sitaki (Nakesha)
Ya nini kuumia bora nile dawa (Nakesha)

Mapenzi sitaki (Nakesha)
nakesha...

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2020


Album : Nakesha (Single)


Copyright : (c) 2021


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

D LOVE

Tanzania

D Love also known as D Love Afrika is a Bongo Flava artist from Tanzania. ...

YOU MAY ALSO LIKE