Nakesha Lyrics

Moyo umekua sugu hadi maumivu yanadunda
Siogopi waongo sipokei
Wakweli mapenzi yamenifunza
Tamu imekua chungu moyo ulifanywa punda
Hadi mizigo ya kokoto
Ikanichosha mwili machozi nikafuta
Sio kama siogopi kuumia tatizo nishaumia sana
Mapenzi ya maharamia nikachukia ujana
Kuna muda nawaza rudia tatizo nikipenda sana
Ndo nafasi wanaitumia kuniumiza mchana
Na usiku usingizi sipati, nakesha
Usiku nalia bahati sina (Nakesha)
Bora pombe mapenzi sitaki (Nakesha)
Ya nini kuumia bora nile dawa (Nakesha)
Kila napotarajia nitafurahia
Ndo nazisisha
Maumivu kwa ndani mwili umekufa ganzi
Kila pendo naloingia
Yanajirudia kunikatisha
Nikatisha tamaa mnyonge mwana simanzi
Kama ningeliweza kuchagua
Utotoni ningeamua
Bora hata nisingeyajua
Yataniua mapenzi
Sio kama siogopi kuumia tatizo nishaumia sana
Mapenzi ya maharamia nikachukia ujana
Kuna muda nawaza rudia tatizo nikipenda sana
Ndo nafasi wanaitumia kuniumiza mchana
Na usiku usingizi sipati (Nakesha)
Usiku nalia ah, bahati sina (Nakesha)
Bora pombe mapenzi sitaki (Nakesha)
Ya nini kuumia bora nile dawa (Nakesha)
Mapenzi sitaki (Nakesha)
nakesha...
WATCH VIDEO
ABOUT THIS SONG
Release Year : 2020
Album : Nakesha (Single)
Copyright : (c) 2021
Added By : Huntyr Kelx
SEE ALSO
AUTHOR
D LOVE
Tanzania
D Love also known as D Love Afrika is a Bongo Flava artist from Tanzania. ...
YOU MAY ALSO LIKE