Home Search Countries Albums

Nafasi Nyingine

JOEL LWAGA

Nafasi Nyingine Lyrics


Mavumbi umenifuta yote
Habari umebadili yote
Machozi umenifuta yote
Aibu umeondoa yote

Umeniita mwana niliyekuwa mtumwa
Umenisimamisha katika wingi wa neema
Na umeniketisha mahali pa juu sana

Ninaucheka wakati uliopita
Nikiufurahia ule ujao
Ninaucheka wakati uliopita
Nikiufurahia ule ujao

Maana umenipa(Nafasi nyingine)
Umenipenda tena bila kukoma(Nafasi nyingine)
Neema yako imeniinua tena(Nafasi nyingine)
Umenipa tena bila kuchoka(Nafasi nyingine)

Mungu wa neema 
Wa neeema(Aaah)
Wa neema, neema (Aaah)
Wa neema, neema (Aaah)
Wa neema, neema (Aaah)

Madaktari walisema sitapona tena
Walimu walisema nitafeli 
Ndugu na jamaa walisema nimeshindikana
Na kumbe wewe waniwazia mema

Umri uliposogea walisema ndoa si fungu langu
Nilipofiwa na mpendwa yule walisema sitaweza tena
Baada tu ya kufilisika, sikumwona wa kuniombea
Na kumbe ndani yao walifurahi niliyopitia

Ninaucheka wakati uliopita
Nikiufurahia ule ujao
Ninaucheka wakati uliopita
Nikiufurahia ule ujao

Maana umenipa(Nafasi nyingine)
Umenipenda tena bila kukoma(Nafasi nyingine)
Neema yako imeniinua tena(Nafasi nyingine)
Umenipa tena bila kuchoka(Nafasi nyingine)

Mungu wa neema 
Wa neeema(Aaah)
Wa neema, neema (Aaah)
Wa neema, neema (Aaah)
Wa neema, neema (Aaah)

Maana umenipa(Nafasi nyingine)
Kweli umenipa(Nafasi nyingine)
Umenipa(Nafasi nyingine)
Bwana umenipa(Nafasi nyingine)

Mungu wa neema 
Wa neeema(Aaah)
Wa neema, neema (Aaah)
Wa neema, neema (Aaah)
Wa neema, neema (Aaah)

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2019


Album : Nafasi Nyingine (Single)


Copyright : (c) 2019


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

JOEL LWAGA

Tanzania

Joel Lwaga is a gospel artist from Tanzania. ...

YOU MAY ALSO LIKE