Home Search Countries Albums

Nimeyumba

BRIGHT

Nimeyumba Lyrics


Miaka tisa Dar, mambo yamefeli
Sina hata bajaji
Eti niuze mkaa ila sio kweli
Mbona sina mtaji

Nanga imepaa nawaza ukabaji
Ili nikidhi mahitaji
Yote yanakataa
Naogopa utapeli nitafungwa

Mara Bright siku hizi hatubambi
Toka amwagwe na management
Anachoimba sisi hatutaki
Anayoyafanya haeleweki

Aliniambia mama, mama 
Mwanaume kupambana nisichoke
Kuna mengi ya kufanya, fanya
Hata nikianguke niinuke

Tena alisema mama, mama 
Cha mtu sumu nisiguse
Kama imeshindikana, kana
Nirudi nyumbani nisilazimishe

Nimeyumba, nimeyumba
Nimeyumba, nimeyumba
Nimeyumba, nimeyumba

Wako wapi wale walosema
Kwamba ni shabiki wa damu
Tena walishika bango
Whatsapp wakaunga team

Redio hawapigi hata ngoma
Maisha yamekuwa magumu
Sina show mapromoter tena
Hawapigi hata simu

Au tayari ndo tayari
Nilowakuta warejee ndani
Stress zinilaze chali
Niwe kulewa dawa kali

Au tayari ndo tayari
Nilowakuta warejee ndani
Stress zinilaze chali
Niwe kulewa dawa kali

Aliniambia mama, mama 
Mwanaume kupambana nisichoke
Kuna mengi ya kufanya, fanya
Hata nikianguke niinuke

Tena alisema mama, mama 
Cha mtu sumu nisiguse
Kama imeshindikana, kana
Nirudi nyumbani nisilazimishe

Nimeyumba, nimeyumba
Nimeyumba, nimeyumba
Nimeyumba, nimeyumba

Amesahaulika Juma Nature
Yuko wapi Inspekta
Atakayeumiza nesi hamtaki kabisa
Ona PNC Tonya mbili
Malovi hambembelezi tena
Bwana misosi, MarTi
Afande tena simba hang'ati tena
Wameyumba

Chelea Mani, Dazi baba
Ferooz wa starehe, wameyumba
20 percenti yule Sparki simwoni pasha ee
Wameyumba

Kila kibanda cha simu Sogi dogi
King Prais ke
Wapi Stara Tomasi Sista P eeh
Wameyumba
Dume bwege kaka Bushoke 
Eeh ameyumba
Baraka the Prince

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2021


Album : Nimeyumba (Single)


Copyright : (c) 2021


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

BRIGHT

Tanzania

...

YOU MAY ALSO LIKE