Home Search Countries Albums

Daktari

WYSE

Daktari Lyrics


Uzuri wako asumini
Asumini napenda ukichanua
Mizunguko kama feni
Feni mbovu chumbani wanipepea

Una maadili, umefunzwa umefunzika
Sifa wastahili, kwako nafaidika
Sihitaji darubini, darubini
Mazuri kukupimia

Hawajui unayonipa mie
Penzi lako maridhawa
Oooh hawajui acha nining'inie
Mapigo yangu ya moyo we ndo dawa

Daktari wee, daktari, unajua dozi yangu
Daktari wee, daktari, ooh tibu maradhi yangu
Daktari wee, daktari, bingwa wa hisia zangu
Daktari wee, daktari, basi nipe mambo yangu

Nikichechemea unaniwaza
Unanipa nguvu ya kuamka kesho
Unanipokea na vizawadi vidogo vidogo
Vyote kwako wewe ni special

Nimegubikwa na furaha, nyota yangu inang'aa
Pete yangu umevaa usije ivue
Usijekukata tamaa, vijineno vya mtaa
Ukajikuta umevivaa usinitue

Hawajui unayonipa mie
Penzi lako maridhawa
Oooh hawajui acha nining'inie
Mapigo yangu ya moyo we ndo dawa

Daktari wee, daktari, unajua dozi yangu
Daktari wee, daktari, ooh tibu maradhi yangu
Daktari wee, daktari, bingwa wa hisia zangu
Daktari wee, daktari, basi nipe mambo yangu

Oooh oooh, ayee eeh
Sasambu sasambua
Sasambu sasambua
Sasambu sasambua mama wee

Oooh oooh, ayee eeh
Sasambu sasambua
Sasambu sasambua
Sasambu sasambua mama wee

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2020


Album : Daktari (Single)


Copyright : (c) 2020


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

WYSE

Tanzania

Wyse is a singer/songwriter from Tanzania. ...

YOU MAY ALSO LIKE