Home Search Countries Albums

Usichelewe

WALTER CHILAMBO

Read en Translation

Usichelewe Lyrics


Aaaah

Walter tenaaa

Mungu wangu

naomba niongee na wewe

Hata kidogo

Nasikia uchungu ndani ya Moyo

Mambo yamekuwa mazito

Na siwezi peke yangu

Naona maumivu ndani ya moyo

Na umesema walipo wawili wewe upo

Najiuliza nikiwa peke yangu je we upo?

Ni kweli na imani

Lakini kuna muda nachoka

Na si kwamba sikuamini

Nakuamini sanaa

Nimeomba,nimefunga na nimetoa sadaka

Ila mambo yanayumba,fanya hima uje haraka

Basi uniambie mi (Ni wapi nakosea)

Baba uniambie mi (Niwapi nakosea)

Yesu uniambie eehh (Niwapi nakosea)

Baba uniambie Mi niwapi nakosea nakuomba

usichelewe...( nachoka, nachoka )

usichelewe...( tazama moyo umechoka )

usichelewe...( nitangoja, ntangoja )

usichelewe...( Mi mwanao bado ntangoja )

Wenzangu wana marafiki

Wa kuwaambia shida zao

Na mimi we ndio wangu RAFIKI

Ninakuambia haja zangu

Siulisema

Utanibariki mjini na mashambani

Siulisema

Niingiapo na nitokapo nitabarikiwa

Siulisema

Fedha na dhahabu vyote ni mali yako

Siulisema

Nikiomba utanipa zaidi ya niombavyo

Nimeomba,nimefunga na nimetoa sadaka

Ila mambo yanayumba,fanya hima uje haraka

Basi uniambie mi (Ni wapi nakosea)

Baba uniambie mi (Niwapi nakosea)

Yesu uniambie eehh (Niwapi nakosea)

Baba uniambie Mi niwapi nakosea nakuomba

usichelewe...( nachoka,nachoka )

usichelewe...( tazama moyo umechoka )

usichelewe...( nitangoja ,ntangoja )

usichelewe...( Mi mwanao bado ntangoja )

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2025


Album : (Single)


Added By : Farida

SEE ALSO

AUTHOR

WALTER CHILAMBO

Tanzania

WALTER CHILAMBO  is a Gospel Singer and Song Writer from Tanzania. He was the winner at Epic Bo ...

YOU MAY ALSO LIKE