Yalah Lyrics
(Ayolizer)
Nimesadiki ya wahenga
Penzi lina raha yake
Mzigo kwa tenga
Imfaacho mtu chake
Denge nimekatwa ngenga
Ah umate mate
Najinyenga nyenga
Mao mao maotate
Huwaga sioni
Ninavyoipanda milima
Ulimi sikioni
Mwili wote wanizizima
Mwenzenu sioni
Macho mawili yote sina
Tunaanza jikoni
Mpaka varandani twalilima
Yalah! yalah yalah, yalah yalah
Oooh yalah yalah yalah yalah
Penzi limenizidia, yalah yalah
Ni kubwa, yalah yalah
Zito, yalah yalah, yalah yalah
Tungezaliwa zamani
Ningesema penzi toga
Tulinywe kibarazani
Tukitafuna maboga
Nimekipanda uani
Kibustani cha uyoga
Tukishiba biryani
Baby tule mboga mboga
Sasa polisi wa nini?
Nikikosa nikamate wewe
Mahakama ya nini?
Nikikosa nihukumu wewe
Penzi chupa la Balindi
Tuligide baby hadi tulewe
Videge shorwe vya nini?
Kifaranga we nibebe mwewe
Huwaga sioni
Ninavyoipanda milima
Ulimi sikioni
Mwili wote wanizizima
Mwenzenu sioni
Macho mawili yote sina
Tunaanza jikoni
Mpaka varandani twalilima
Yalah! yalah yalah (Yalah yalah) yalah yalah
(Yalah yalah) Yalah yalah yalah yalah
Penzi limenizidia, yalah yalah
Ni kubwa, yalah yalah
Zito, yalah yalah, yalah yalah
WATCH VIDEO
ABOUT THIS SONG
Release Year : 2021
Album : Definition of Love (Album)
Copyright : (c) 2021 WCB Wasafi.
Added By : Huntyr Kelx
SEE ALSO
AUTHOR
MBOSSO
Tanzania
MBOSSO Khan (real name Mbwana Yusuph Kilungi born 3rd October 1991) is an artist | ...
YOU MAY ALSO LIKE