Accueil Recherche Pays Albums

Kampeni Lyrics


Waliponikaribia na kuniaibisha eeh
Haukunyamaza ukanipigania eeh
Waliponivua utu na kulichana vazi langu
Na heshima ulinikumbatia nisiaibike

Waliposema mi mjinga, ujinga ninao
Sababu hekima haiezi bila upendo
Nilipoyafunika madhaifu yao
Na kumbe tafsiri ni mjinga kwao

Hata nilipokaa kimya wewe uliona yote
Uliponyamaza hukuacha nife
Ninakushukuru ooh, ooh Jire Dumo
Asante, ooh, oooh Igwe

Nitafanya kampeni za wema wako
Wajue Mungu ni mwema
Nitafanya kampeni za wema wako
Wajue Yesu ni mwema

Unaponibariki bariki adui zangu
Ili wasinisonge kutaka uhai wangu
Unapopiga mapigo samehe rafiki zangu
Wanaoning'ata alafu wanapuliza puu

Hata nilipokaa kimya wewe uliona yote
Uliponyamaza hukuacha nife
Ninakushukuru ooh, ooh Jire Dumo
Asante, ooh, oooh Igwe

Nitafanya kampeni za wema wako
Wajue Mungu ni mwema
Nitafanya kampeni za wema wako
Wajue Yesu ni mwema

Fadhili zako zadumu kila asubuhi
Wewe ni Mungu unayesimamisha mianga angani
Pendo lako lanitosha daima
Huruma yako imepita fahamu zangu
Ninakupenda Yesu, ninakupenda mwamba wangu

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2021


Album : Kampeni (Album)


Copyright : (c) 2021


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

GOODLUCK GOZBERT

Tanzanie

Goodluck Gozbert est un artiste chanteur de musique Gospel d'origine Tanzanienne. ...

YOU MAY ALSO LIKE