Nikumbushe(Cover) Lyrics

Ninahisi kinywa kujawa na lawama tele
Pale mambo yanapoonekana hayaendi
Ni ajabu sana namna moyo unahangaika(Natafuta majibu)
Ajabu sana moyo unapoonyesha mashaka
Ya kwamba japo kuwa Mungu
Anaishi ndani yangu, kuna muda nahofu
Ya kwamba japo kuwa Mungu
Anaishi ndani yangu, kuna muda nahofu
Oooh nakumbuka wana wa Israeli
Katika bahari la shamu
Japo walikatiza
Katikati ya bahari kwa ushindi
Kwa nyimbo nyingi
Waliimba na kumsifu Bwana
Lakini baada ya kuvuka na kuliona jangwa
Yalibadilika mambo
Manung'uniko yalisimama aah
Na kusahau muujiza alotenda bwana mwanzo
Aaah...
Eeeh Mungu nisaidie eeh eeh eeh, oooh
Nikumbushe wema wako nisije laumu
Nikumbushe ukuu wako wakati wa magumu
Nikumbushe shuhuda zako ili nikusifu
Niimbe wimbo wa sifa
Katikati ya machozi
Niimbe wimbo wa sifa
Katikati ya machozi eeh eh
Eh Mungu nisaidie
Nisaidie kukumbuka Baba
Ya kwamba umenichora kiganjani mwako
Kati ya wengi waliopo duniani
Na mimi umeniona oooh..
Nikumbushe bwana kwamba ni wewe
Unaniponya ninapoumwa
Kwamba ni wewe
Mlipaji wa ada yangu shuleni oooh..
Yakwamba kama umeniacha hatua moja
Nisingelifika mahali nilipo
Eeeh Baba, umeniukung'uta mavumbi
Kung'uta mavumbi mimi na kuniheshimisha oooh..
Nikumbushe wema wako nisije laumu
Nikumbushe ukuu wako wakati wa magumu
Nikumbushe shuhuda zako ili nikusifu
Niimbe wimbo wa sifa
Katikati ya machozi
Niimbe wimbo wa sifa
Katikati ya machozi eeh eh
WATCH VIDEO
ABOUT THIS SONG
Release Year : 2019
Album : Nikumbushe(Cover) (Single)
Copyright : (c) 2019 Afro Covers.
Added By : Huntyr Kelx
SEE ALSO
AUTHOR
YOU MAY ALSO LIKE