Home Search Countries Albums

Daima Mkenya

ERIC WAINAINA

Read en Translation

Daima Mkenya Lyrics


Umoja ni fahari yetu
Undugu ndio nguvu
Chuki na ukabila
Hatutaki hata kamwe
Lazima tuungane, tuijenge nchi yetu
Pasiwe hata mmoja
Anaetenganisha

Naishi, natumaini
Najitolea daima Kenya
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu

Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

Kwa uchungu na mateso
Kwa vilio na huzuni
Tulinyakuliwa Uhuru
Na mashujaa wa zamani
Hawakushtushwa na risasi
Au kufungwa gerezani
Nia yao ukombozi
Kuvunja pingu za ukoloni

Naishi, natumaini
Najitolea daima Kenya
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu

Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

Wajibu wetu
Ni Kuishi kwa upendo
Kutoka ziwa mpaka pwani
Kaskazini na kusini

Naishi, natumaini
Najitolea daima Kenya
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu

Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2015


Album : Daima Mkenya (Single)


Copyright : (c) 2020


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

ERIC WAINAINA

Kenya

Eric Wainaina is an artist from Kenya. He is best known for his partriotic songs for Kenyans. ...

YOU MAY ALSO LIKE