Home Search Countries Albums

Cha Unyonge

ALLY MAHABA

Cha Unyonge Lyrics


Umaarufu wako ungeupata wapi
Kama sio mimi kukutangaza
Kujisifu kwako, kutakufikisha wapi
Hio bahari ina mashaza

Usione siongei
Vituko vyako mi naviona
Nyuma sirejei
Ulipopachana nishapashona

Wala sikuongopei
Umejazwa maneno maneno maneno
Kuniacha mimi
Tangu ulipopanda bei
Walitoa meno, meno, meno nje
Kunicheka mimi

Kukuvumilia sana
Ipo siku nitapata pia (Maana)
Sitokung'ang'ania
Huko uliko pashike kiukweli

Kweli umenipatia sana
Nimepotea njia (Maana)
Nilikuaminia ukaniziba macho
Ukanitapeli

Nakuombea ulo naye asikuongopee
Kuja kuachwa utalia sana
Wambeya wambeya waogopee
Watakuponza utalia sana sana sana

Nimeuponza, nimeuponza
Nimeuponza wangu moyo
Nimeuponza, nimeuponza
Nimeuponza wangu moyo

Kinyago nakichonga mwenyewe
Kimenitisha aah
Kama kifaranga kaninyakua mwewe
Nimekwisha aah

Hivyo visnap, mashauzi
Navi emoji vya mdomo upande kunikomoa
Kwenye Whatsapp siulizi
Unatupia vipande pande, vya kuniua

Kuna leo na kesho 
Hao wanaokupa ujasiri
Wa kunisema nisema nisema
Vishindo vina mwisho
Sina pupa unafikiri
Kukujibu mapema mapema mapema

Nije na matarumbeta (Na)
Nikutoege nishai (Na)
Mwishowe si tutateta (Wee)
Sio zangu mimi wee

Unawatuma wacommenti (Na)
Wanichambe kila posti (Na)
Wanakesha kwenye neti (Wee)
Sio zangu mimi wee

Nakuombea ulo naye asikuongopee
Kuja kuachwa utalia sana
Wambeya wambeya waogopee
Watakuponza utalia sana sana sana

Nimeuponza, nimeuponza
Nimeuponza wangu moyo
Nimeuponza, nimeuponza
Nimeuponza wangu moyo

Nimeuponza, nimeuponza
Nimeuponza wangu moyo
Nimeuponza, nimeuponza
Nimeuponza wangu moyo

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2021


Album : Cha Unyonge (Single)


Copyright : (c) 2021


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

ALLY MAHABA

Kenya

Ally Mahaba is an artist from Kenya signed under ATL MUSIC. ...

YOU MAY ALSO LIKE