Tutazame Kule Mbele Lyrics

Tutazame kule mbele, asubuhi inakuja
Tuamini Mungu wetu, atafanya kazi yake
Kufukuza mashetani, kumiliki nchi yote
Tutashinda tukiomba, Mungu anatusikia
Tutashinda tukiomba, Mungu anatusikia
Tutashinda tukiomba, Mungu anatusikia
Tutashinda tukiomba, Mungu anatusikia
Tarumbeta linalia, tuamke wote sasa
Mungu wetu anataka sisi sote tutakaswe
Kila mtu awe safi katika kanisa lake
Uliache nung’uniko, utapata nguvu yake
Uliache nung’uniko, utapata nguvu yake
Uliache nung’uniko, utapata nguvu yake
Hima ninyi, watu wake
Bwana yu pamoja nasi
Tutashinda majaribu kwa uwezo wake Yesu
Twende tumhudumie kwa kumpa mali yake
Hata roho na akili zimtumikie Bwana
Hata roho na akili zimtumikie Bwana
Hata roho na akili zimtumikie Bwana
Watu wengi hawajui njia yakufika mbingu
Wanakuwa wamefungwa kwa mikono ya shetani
Twende tukawatafute, tuwavute kwa mwokozi
Na kuomba na kukesha hata kuja kwake Yesu
Na kuomba na kukesha hata kuja kwake Yesu
Na kuomba na kukesha hata kuja kwake Yesu
Na kuomba na kukesha hata kuja kwake Yesu
WATCH VIDEO
ABOUT THIS SONG
Release Year : 2023
Album : Tutazame Kule Mbele (Single)
Added By : Penuel Gospel Singers
SEE ALSO
AUTHOR
YOU MAY ALSO LIKE