Usilie Lyrics

Asubuhi imetimu, kumepambazuka
Kumekucha salama
Shida zinatulazimu haraka kuinuka
Kutafuta vya ngama
Namuona mama ameshika tama
Namuona baba amekata tamaa
Jirani yangu anaumwa sana
Kila kukicha afadhali ya jana
Usilie baba, usilie mama
Ah usilie dada futa machozi
Usilie kaka, usilie rafiki
Ah usilie ndugu futa machozi
Yametawala mawazo
Na kila mara vikwazo
Ila changamoto ni funzo
Usikate tamaa
Taabu zinaturudia ila
Nguzo ni kuvumilia pia
Ushindi unakaribia tia
Dunia wee ee
Namuona dada ameshika tama
Namuona kaka amekata tamaa
Rafiki zangu wanashida sana
Kila kukicha afadhali ya jana
Usilie baba, usilie mama
Ah usilie dada futa machozi
Usilie kaka, usilie rafiki
Ah usilie ndugu futa machozi
Usilie, oooh aah
Na usikate tamaa
Tururutu....
Muda unakuja, na muda unafika
Usilie, don't don't cry
You don't cry, you don't cry
Inuka tena
(Free Nation)
WATCH VIDEO
ABOUT THIS SONG
Release Year : 2020
Album : Usilie
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
SEE ALSO
AUTHOR
YOU MAY ALSO LIKE