Home Search Countries Albums

Nisaidie

FRED MSUNGU

Nisaidie Lyrics


Mateso yakizidi, hofu hutawala
Hakuna tumaini, lini yatakwisha?
Imani yatoweka, hakuna tumaini
Mungu wangu nisaidie

Hakuna hata mmoja aniwazie mema
Adui wamezidi rafiki wageuka
Sioni hata mmoja wa kunisaidia
Baba wewe, Mungu wangu nisaidie

Ninapoonewa ninapolemewa
Giza likitanda 
Nguvu zikiisha
Mungu wangu nisaidie

Nakungoja wewe nipe nguvu mpya
Nipeperuke kama tai nitembee bila choka
Nipige mbio mbele bila kuzimia
Mungu wangu nisaidie

Nimeshajinyonyoa manyoya
Nimeparua kucha kwa amani
Nimepunguza uzito wa mwili
Niko tayari kuruka tena

Maisha yangu ya pili mazuri
Kulinganisha na yale ya kwanza
Niko tayari ninazo nguvu
Kama tai

Ujana wangu umerejea
Maisha yangu yamerejea
Sasa niko na nguvu 
Sionewi tena

Ninapoonewa ninapolemewa
Giza likitanda 
Nguvu zikiisha
Mungu wangu nisaidie

Nisaidie,nisaidie
Nisaidie, nisaidie

Wale wamngojao Bwana
Watapata nguvu mpya
Watapaa juu kwa mbali
Kama tai oooh

Ninapoonewa ninapolemewa
Giza likitanda 
Nguvu zikiisha
Mungu wangu nisaidie
Mungu wangu nisaidie

Ninapoonewa ninapolemewa
Giza likitanda 
Nguvu zikiisha
Mungu wangu nisaidie
Mungu wangu nisaidie

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2019


Album : Nisaidie (Single)


Copyright : (c) 2019


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

FRED MSUNGU

Tanzania

Fred Msungu is a pastor , author and the founder of Pure mission (Tanzania ) Other aspects of Fred&# ...

YOU MAY ALSO LIKE