Nikuache Lyrics

Haaa haa.. (Shirko Media)
Najiona najiuliza
Kwa nini macho yangu mekundu
Kwa taarifa yako nimetoka kulia
Hivi utaniumiza hadi lini
Litundu la moyo wangu
Mie mwenzako nipate tulia
Japo moyoni, moyoni
Nimejawa na subira, subira
Kuishi na wewe imekuwa kazi
Naona kama inashindikana kweli
Kama siyaoni vile, inanitia hasira
Madhila wanifanyia wazi
Kuishi nawe mi naona nishafeli
Nichambane na madem wako
Japo mi huwaga sishiki simu yako
Hivi kwa nini hawatosheki kwako
Waniandame mie
Kunigombeza we ndio zako
Kisa tu naishi kwako
Ushashukisha thamani yako
Kwangu mie
Dawa dawa yako nikuache
Nijiweke mbali nawe
Sawa sawa yako nikuache
Kama mawingu na mawe
Dawa dawa yako nikuache
Penzi lako kaligawe
Sawa sawa yako nikuache
Mi utaniumizaa
Kama kufumania nimekufumania
Sana na Tiffah nikakusamehe, haijatosha
Kusudi unarudia tena kwa kutia nia
Naona sifa mwanamume, umenichosha
Sina jeuri ya kujibu mi najiliza
Mapungufu yangu bubu nakusikiza
Hunaga cha taratibu wakandamiza
Mwanamume una gubu kupitiliza
Nichambane na madem wako
Japo mi huwaga sishiki simu yako
Hivi kwa nini hawatosheki kwako
Waniandame mie
Kunigombeza we ndio zako
Kisa tu naishi kwako
Ushashukisha thamani yako
Kwangu mie
Dawa dawa yako nikuache
Nijiweke mbali nawe
Sawa sawa yako nikuache
Kama mawingu na mawe
Dawa dawa yako nikuache
Penzi lako kaligawe
Sawa sawa yako nikuache
Mi utaniumizaa
Dawa dawa yako nikuache
Nijiweke mbali nawe
Sawa sawa yako nikuache
Kama mawingu na mawe
Dawa dawa yako nikuache
Penzi lako kaligawe
Sawa sawa yako nikuache
Mi utaniumizaa
WATCH VIDEO
ABOUT THIS SONG
Release Year : 2020
Album : Nikuache
Copyright : (c) 2020 Shirko Media.
Added By : Huntyr Kelx
SEE ALSO
AUTHOR
AKEELAH
Kenya
Akeelah is an artist from Mombasa, Kenya. Signed under Shirko Media Entertainment. ...
YOU MAY ALSO LIKE