Kwaru Lyrics

(Ayolizer)
Mmmh aaah aah, mmmh aaah
Aaaah, aah
Roho ingekuwa na macho ungejionea
Moyo haufanyi kificho ukiotea
Mimi kifigiso nacho ungeongea
Mwili wangu rojorojo nanyong'onyea
Chungu nilichopika wamepakua wenzangu
Huruma napokutishwa wamechukua wezangu
Na kitabu chetu cha mapenzi
Kurasa wamechanachana
Hazisomeki tena tenzi
Vimepoteza maana
Mpofu moyo wangu
Ulishindwa ona
Hukuandikwa wa kwangu
Limenikaba nalitema
Kwaru kwa kwaru kwaru
Kachukua kisu ye anaukwarua
Kwaru kwa kwaru kwaru
Moyo wangu unaumia
Kwaru kwa kwaru kwaru
Ye kwa nguvu anaukwarua
Kwaru kwa kwaru kwaru
Jamani moyo wangu unaumia
Eeh langu tatizo
Nachuna najimaliza
Mi nakesha kumwaza
Naweweseka lake jina, ooh jina
Oooh basi kwa unyonge
Najikaza niache kulia
Maana kwake bahati sina, ooh sina
Maumivu ameipora furaha yangu
Oooh amekwenda nayo
Na zangu mbivu zimeniozea
Hasara kwangu, yatapita hayo
Mpofu moyo wangu
Ulishindwa ona
Hukuandikwa wa kwangu
Limenikaba nalitema
Kwaru kwa kwaru kwaru
Kachukua kisu ye anaukwarua
Kwaru kwa kwaru kwaru
Moyo wangu unaumia
Kwaru kwa kwaru kwaru
Ye kwa nguvu anaukwarua
Kwaru kwa kwaru kwaru
Jamani moyo wangu unaumia
WATCH VIDEO
ABOUT THIS SONG
Release Year : 2020
Album : I am Zuchu EP / Kwaru (EP)
Copyright : (c) 2020 Wasafi Records.
Added By : Huntyr Kelx
SEE ALSO
AUTHOR
ZUCHU
Tanzania
Zuchu real name Zuhura Othman Soud Kopa (born November 22, 1993) is an artist/Singer/Songwriter/Perf ...
YOU MAY ALSO LIKE