Home Search Countries Albums

Kwaru

ZUCHU

Kwaru Lyrics


(Ayolizer)

Mmmh aaah aah, mmmh aaah
Aaaah, aah

Roho ingekuwa na macho ungejionea
Moyo haufanyi kificho ukiotea
Mimi kifigiso nacho ungeongea
Mwili wangu rojorojo nanyong'onyea

Chungu nilichopika wamepakua wenzangu
Huruma napokutishwa wamechukua wezangu

Na kitabu chetu cha mapenzi
Kurasa wamechanachana
Hazisomeki tena tenzi 
Vimepoteza maana

Mpofu moyo wangu
Ulishindwa ona
Hukuandikwa wa kwangu
Limenikaba nalitema

Kwaru kwa kwaru kwaru
Kachukua kisu ye anaukwarua
Kwaru kwa kwaru kwaru
Moyo wangu unaumia

Kwaru kwa kwaru kwaru
Ye kwa nguvu anaukwarua 
Kwaru kwa kwaru kwaru
Jamani moyo wangu unaumia

Eeh langu tatizo
Nachuna najimaliza
Mi nakesha kumwaza
Naweweseka lake jina, ooh jina

Oooh basi kwa unyonge 
Najikaza niache kulia
Maana kwake bahati sina, ooh sina

Maumivu ameipora furaha yangu
Oooh amekwenda nayo
Na zangu mbivu zimeniozea
Hasara kwangu, yatapita hayo

Mpofu moyo wangu
Ulishindwa ona
Hukuandikwa wa kwangu
Limenikaba nalitema

Kwaru kwa kwaru kwaru
Kachukua kisu ye anaukwarua
Kwaru kwa kwaru kwaru
Moyo wangu unaumia

Kwaru kwa kwaru kwaru
Ye kwa nguvu anaukwarua 
Kwaru kwa kwaru kwaru
Jamani moyo wangu unaumia

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2020


Album : I am Zuchu EP / Kwaru (EP)


Copyright : (c) 2020 Wasafi Records.


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

ZUCHU

Tanzania

Zuchu real name Zuhura Othman Soud Kopa (born November 22, 1993) is an artist/Singer/Songwriter/Perf ...

YOU MAY ALSO LIKE