Home Search Countries Albums

Nitasubiri

ZABRON SINGERS

Nitasubiri Lyrics


Ya nini Mungu kujificha wakati wa shida?
Wakati mwingine kama kweli huoni
Wajua yote yalonikuta hasimliki
Nimelia na kujinyamazisha pekee yangu

Moyoni nikataabika, furaha ikaenda
Sikumwona wa kumwelezea shida
Rafiki pekee namwamini, ni Yesu mfariji
Ndio maana sijamwambia mtu shida zangu

Nitasubiri na kusubiri sitachoka
Nimeshamezana na wewe kwa maombi
Usipojibu, au ujibu nitaelewa
Nashukuru, hata kwa majaribu
Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Nitasubiri na kusubiri sitachoka
Nimeshamezana na wewe kwa maombi
Usipojibu, au ujibu nitaelewa
Nashukuru, hata kwa majaribu
Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Kwa nini sasa umesimama mbali nami Bwana?
Muda mwingi mi najihisi mi ni mpweke
Jidhihirishe mi nikuone, nakuhitaji Bwana
Nibariki sasa ukijibu maombi, yangu

Najua mengi nimekuudhi, nimetenda dhambi
Ndio maana ukasimama mbali nami
Nisamehe yote yote bure, kwa damu ya Yesu
Nifanye mi niwe mtoto wako siku, zote

Nitasubiri na kusubiri sitachoka
Nimeshamezana na wewe kwa maombi
Usipojibu, au ujibu nitaelewa
Nashukuru, hata kwa majaribu
Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Nitasubiri na kusubiri sitachoka
Nimeshamezana na wewe kwa maombi
Usipojibu, au ujibu nitaelewa
Nashukuru, hata kwa majaribu
Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2019


Album : Mkono wa Bwana (EP)


Copyright : (c) 2021


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

ZABRON SINGERS

Tanzania

Zabron singers is an evangelism group found in Kahama Tanzania, since 2006 to 2015 more than sixty h ...

YOU MAY ALSO LIKE