Home Search Countries Albums

Nenda Salama MAGUFULI Lyrics


Tunabaki na picha maneno ya kimaza
Hivi kweli umeondoka baba 
Au ukute naota labda eeh

Kweli umetuheshimisha
Juhudi matendo yako
Hivi kweli umeondoka baba 
Au ukute naota labda eeh

Imekuwa ngumu kuamini
Tunayempenda hatutamwona
Tunayempenda hayuko nasi tena

Imekuwa mapema hivi kwanini
La mwisho baba hata ungesema
Namwomba Mungu ulale mahali pema

Na asiyejua umuhimu, umuhimu wako baba
Atasherehekea kwa uvivu, uvivu wa fikra zake
Umeondoka mwalimu ingawa kifo ni ibada
Hayazoeleki maumivu

Baba umeondoka, umeondoka umetuacha
We nenda salama 
Baba umeondoka, umeondoka umetuacha
We nenda salama 

Japo Doctor umesha speech kuhusu uchumi wa kati
Wapo waliokudhihaki
ulipopambana na wale wengi walioidhulumu haki
Zile ngumu nyakati haukuwa na wasiwasi
OMG I can't believe leo umekuwa hayati

Si ni vigumu kutadhmini ila haina walakini
Kumpoteza aliyejisacrife kisa masikini
Aliweka kando umimi akafanya mambo mengi kwa usawa
Bila hata kujali kabila wala dini

Kweli binadamu wa sasa muda wetu ni mchache baba
Muda wetu ni mchache labda
Ukipata ata wasaa wa mwisho tupe neno la uzalendo
Labda kichwani mwetu ingebaki --

Baba umeondoka, umeondoka umetuacha
We nenda salama 
Baba umeondoka, umeondoka umetuacha
We nenda salama 

Yo baba mambo mengi umefanya
Kutumbua viongozi walopita njia za panya
Umeondoka baba nchi umeiacha salama
Ulazwe mahali pema japo mapema sana

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2021


Album : Nenda Salama MAGUFULI (Single)


Copyright : (c) 2021 Too Much Money (TMT)


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

WHOZU

Tanzania

Whozu Andaskoo is a musician from Tanzania. ...

YOU MAY ALSO LIKE