Home Search Countries Albums

Wanyabi Cypher (New Year Chapter)

WANYABI Feat. OKA MARTIN

Wanyabi Cypher (New Year Chapter) Lyrics


[Bashoo]
Asante kunifanya niwe imara
Uliyebadili mlingoti dhaifu kuwa imara
Mlinzi wa roho yangu unayekesha mi nikilala
Maana wanangu wa faida ndo wananitiaga hasara

Sa wako wapi tuliwaamini wakatusaliti
Wengine walijifanya wanaharakati
Kumbe wazandiki wanatupiga busu la unafiki
Wakila hupewi kijiko labda kisu na maji

Wewe Mungu uliyefanya leo ikawa
Mwarubaini mchungu ukaufanya ni dawa
Cheki wanatupa ndugu wanakumbatia chawa
Ulale pema bibi nesi mi niko sawa

Mungu Baba naomba ibariki na serikali
Wape akili na mabinti wanaojiita pisi kali
Maana maisha ni safari, una mwisho huu
Nina kauli ndo mlango wa kuingilia mbinguni

[Carpoza]
Naishi kuwa peaceful na nina happy
Hajanipa mkwanja ka Ginimbi niko flashy
Mwingi wa huruma Jah ananiona nafsi
Ameniweka safe place kanipa ufamous-i

Kama unafanya basi fanya kwa kuhini though
Kama una zero ukipambana na kumia bro
Mafungu saba mi ndo la kwanza na la pili
Na ukinipa mke mi nataka naichomaga

Ninayekutana naye ana sababu ameshasema
Kila naye achana naye nijifunze unavyosema
Sina gang sina crew peke yako ndo unatosha
Nilikuona pia kaja hawker hii hapa Wanyabi sasa

Eti huwezi achana nayo unazinguaje
Wengine watasema unaiga watohili wacha jo
Wanakuchora ukitoboa tulisema say
Mungu hapendi wanafiki na ndio maana nawachoma mzee

[T Swiga]
Kwa mengi umenitendea nahitaji nikushukuru
Umenipa pumzi bure napumua hunidai ushuru
Sina budi kujirudi hata nisipokosa
Maana kifo hunikumbusha mwosha maiti naye huoshwa

Sitochoka kukuabudu mpaka ipigwe parapanda
Unipokee hio siku nitakuja nimevaa sanda
Usiku kiza mchana mwanga, nyumba mchawi nyumba mganga
We ndo kiboko cha waganga

Mungu wangu mimi mpenda haki
Alipogundua sina wa ubavu
Hakusita kunipa shosti
Kwa dhambi ya udhinifu na akili Mi ni mkosefu
Amenilinda mechi nyingi uwanjani nimecheza peku

Wabariki mashabiki bila nyinyi hakuna mimi
Mungu juu si ni chini ukiomba wizi ye hakunyimi
Yuko peace tu na ninyi, hata uvae saa ya ukutani
Hujui kwake utafika lini

[Oka Martin]
Kalijua jiji, kamekuwa kagwiji
Kanaomba na zigi kanatoa bangi
Dua haziskiki mmekosa misingi
Nyumba ya ibada mnasnap ni upimbi

Hello God sijui ka unajua
Makalio ndio yanaongoza kutusumbua
Mtoto mzuri akiposti commenti mia nane stini
Ila Mnyabi nikiposti ah we nitajilike mimi

Eti wenye hela wanatusema masikini
Cha ajabu nao wanakufa aki ya mama siamini
Hennessy na Bellaire wanaona ndo maisha
Wapumbavu kweli utapata kuwapumzisha

Siku hizi postor kawa mwanasiasa
Anatuchanganya waumini ah we tumedata
Nasubiri safari ya Japani ni utata
Na kuna mmoja kaniambia nikakanyage mafuta

[Cat P]
Na sita pupa ya maisha
Nikijibanza kama Stoney
Huku nikihustle hard pesa iwe kibindoni
Nabangaiza route tu duniani
Poteza pesa ukipoteza maisha tu buriani

I say kazi juu ya kazi nikiunganisha na player
Nafikiri bila Mungu maishani ningepotea
Kazi juu ya kazi sina muda kuchezea
Natafuta pesa we nenda tafuta babycare

Si unajua na mitaa inatufundisha ucomando
Usibishe maana Manzese pia kuna Rambo
Ingekuwa vipi Uncle bila us, devil bila Lot
Ingekuwa vipi father bila son, Tecno bila phone
Ingekuwa vipi country bila people, pete bila kito
Ingekuwa vipi ziwa bila mito yeah

Na zangu shida natatua
Hajai niacha dilemma
Pesa na babe zinaingia kishi bila kudema
So wa kubang kubang bang
Nizame club ung'oe beach mixer kurbang bang
(I'm Out)

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2021


Album : Wanyabi Cypher (New Year Chapter) (Single)


Copyright : (c) 2021


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

WANYABI

Tanzania

Wanyabi a group from East Africa (Tanzania) founded by Oka Martin, Carpoza and Cat P (Mabrich). ...

YOU MAY ALSO LIKE