Home Search Countries Albums

Hatua kwa Hatua

REBEKAH DAWN Feat. MERCY MASIKA

Hatua kwa Hatua Lyrics


Sauti nyingi zinanizingira
Mawaitha mingi, njia nyingi
Lakini najua Sauti moja tu la kufuata
Sina Mchungaji mwingine ila Yesu

Hata wengine wakiteleza njiani
Nitazidi kuwa mwaminifu Kwake
Nitaamini neno Lake
Hajawahi kunipotosha

Hatua kwa hatua, nitaendelea
Mungu mbele yangu, nitamfuata
Hakuna njia ingine najua
Hatua kwa hatua, nitaendelea

Njia zake zaaminika
Neno lake ni la kweli
Kwa hilo nitasimama
Sitainamia dunia
Sina Mwongozo mwingine ila Yesu

Sijawahi ona mwenye haki ameachwa
Waliokuchagua hawajawahi kujuta
Kwa hivyo nitazidii Nawe, hata nisipoelewa

Hatua kwa hatua, nitaendelea
Mungu mbele yangu, nitamfuata
Hakuna njia ingine najua
Hatua kwa hatua, nitaendelea

Oooh, nitakufuata
Nitakufuata Yesu, Kiongozi mwema

Mkombozi, sina mwingine
Mfalme, sina mwingine
Mwenye Enzi, sina mwingine
Msaidizi, sina mwingine
Mponyaji, sina mwingine
Mtetezi, sina mwingine
Mwokozi, sina mwingine
Mfariji, sina mwingine

Hatua kwa hatua, nitaendelea
Mungu mbele yangu, nitamfuata
Hakuna njia ingine najua
Hatua kwa hatua, nitaendelea

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2021


Album : Hatua kwa Hatua (Single)


Copyright : (c) 2021


Added By : Huntyr Kelx

SEE ALSO

AUTHOR

REBEKAH DAWN

Kenya

Rebekah Dawn is a gospel artist, gospel minister, songwriter and creative director at Nairobi L ...

YOU MAY ALSO LIKE