Home Search Countries Albums

Mbagala Lyrics


Busara na upole, na hekima nilorithi kutoka kwa mama yangu, mama
Vyote haukuvijali, ukaona silingani kabisa kuwa na wewe
Ka kuti na mkole, ukakata kabisa na shina la penzi langu nana
Eti kisa mali, ukaona bora uniache mimi na uolewe
Ile siku shekhe namuona anachoma ubani
Unavishwa pete unakuwa mke wa fulani
Nliumia sana, sana
Ile siku shekhe namuona anachoma ubani
Unavishwa pete unakua mke wa fulani
Niliumia sana, niliumia sana, sana

Tatizo kwetu Mbagala, hapa nyumba mbele jalala
Tatizo kwetu Mbagala, ukaona mapenzi siwezi

Ungejua jinsi gani
Machozi nlolia kwa uchungu wa penzi langu na
Mwenzio jinsi gani, vile nimeumia moyoni
Hata kupendwa sitamani
Utamu wa mapenzi mwenzako umekula kwangu ma
Mwenzio sitamaani, hata raha tena mi sioni
Ah naskia hivi sasa una mtoto anaitwa Mamu
Vile akinuna mpaka atabasamu
Mmefanana sana, sana
Mi mwenzako tena mapenzi mi sina hamu
Tena na mpango wa kuhama Dar Es Salaam
Nataka niende mbali, niepuke vita na walimwengu
Mi mwenzenu siwezi

Tatizo kwetu Mbagala, hapa nyumba mbele jalala
Tatizo kwetu Mbagala, ukaona mapenzi siwezi
[Bridge]
Nasema Mbagala, Mbagala, Mbagala aa aaha
Mbagala, ukaona mapenzi siwezi
Nasema Mbagala (Mbagala), Mbagala (Mbagala), Mbagala (Mbagala) ee eh
Mbagala, ukaona mapenzi siwezi

Tatizo kwetu Mbagala, hapa nyumba mbele jalala
Tatizo kwetu Mbagala, ukaona mapenzi siwezi

Enjoy Synced Lyrics With Our Mobile App

Download on Google PlayGet it on App Store

WATCH VIDEO

ABOUT THIS SONG


Release Year : 2013


Album : Diamond Singles (Single)


Copyright : (c)2013


Added By : Trendy Sushi

SEE ALSO

AUTHOR

DIAMOND PLATNUMZ

Tanzania

Naseeb Abdul Juma ( born on 2nd October 1989 ), popularly known by his stage name Diamond Platnumz, ...

YOU MAY ALSO LIKE